MTANGAZAJI

KILICHOFANYIKA SIKU YA MTANZANIA UGHAIBUNI

Picha na Habari za Freddy Macha  

Siku nzima ya Mtanzania lilifana sana wiki iliyopita (Jumapili 30 Juni, 2019), London. Mafanikio ya shughuli yalitokana na ushirikiano wa vichwa vingi badala ya mtu mmoja( au wachache). Hafla ilihudhuriwa na kuhutubiwa rasmi na Balozi wetu Uingereza, Mheshimiwa Asha Rose Migiro. Wenzake karibu wote ofisini pia, walikuwepo na Juma Shah, wa kitengo cha Uhamiaji akachangia kufafanua masuala ya pasipoti mpya. Kila mshiriki alilipa paundi 20 tu ( kama shilingi nusu laki) kiasi kinachowezekana kwa mfanyakazi yeyote Uingereza kupata chakula, vinywaji na kusikia maelezo ya wataalamu mbalimbali asubuhi hadi usiku.

  1- Bango la tukio 
Mbali na Watanzania kuonana, tamasha lilikutanisha maarifa mbalimbali ya kisayansi, biashara, sanaa, nk. Baadhi ya wazungumzaji walirushwa moja kwa moja toka nyumbani kufafanua mada za fedha, uwekezaji, utalii na uchumi. Taswira ilionesha hali muafaka kimaendeleo, Bongo kutokana na uongozi wa Rais John Magufuli. Sehemu mosi ilikuwa majadiliano, ikafuatia sanaa na mitindo; hatimaye, jioni, chakula na densi. Balozi alizungumza mengi ila muhimu alikumbusha Watanzania Ughaibuni kuelekeza ujuzi na uzoefu wetu nyumbani... Dk Migiro : “Tunahitaji taaluma na weledi wenu kwa maendeleo ya  taifa letu..."  6- Mavazi ya All Things African - pic by F Macha, 2019.jpg
               Bidhaa mbalimbali za Kitanzania zilizooneshwa na Wajasiriamali
 16- Wajisiramali- Laila Hamza, Noeta, Anna Lukindo na Sia Travel- pic by F Macha 2019.jpg
Toka kushoto. Wajasiria mali, Laila Hamza, Noeta, Anna Lukindo ( mwendeshaji wa mitindo ya "Anna Luks") na Sia Travel (Biashara ya utalii na mwalimu wa Kiswahili ) 

18- Washiriki wakiwa na Patronella Mlowe (pili toka kushoto- pic by F Macha, 2019.jpgPetronella Mlewa (wa pili kutoka kushoto), anayejishughulisha sana kitaaluma na Watanzania na marafiki zao Uingereza, akiwa na baadhi ya wahudhuriaji.
  19-Mavazi yaliyooneshwa- pic by F macha 2019
Baadhi ya mavazi mengi ya Kitanzania, yaliyooneshwa 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.