KILICHOFANYIKA SIKU YA MTANZANIA UGHAIBUNI
Picha na Habari za Freddy Macha
Siku nzima ya Mtanzania lilifana sana wiki iliyopita (Jumapili 30 Juni, 2019), London. Mafanikio ya shughuli yalitokana na ushirikiano wa vichwa vingi badala ya mtu mmoja( au wachache). Hafla ilihudhuriwa na kuhutubiwa rasmi na Balozi wetu Uingereza, Mheshimiwa Asha Rose Migiro. Wenzake karibu wote ofisini pia, walikuwepo na Juma Shah, wa kitengo cha Uhamiaji akachangia kufafanua masuala ya pasipoti mpya.
Kila mshiriki alilipa paundi 20 tu ( kama shilingi nusu laki) kiasi kinachowezekana kwa mfanyakazi yeyote Uingereza kupata chakula, vinywaji na kusikia maelezo ya wataalamu mbalimbali asubuhi hadi usiku.
![1- Bango la tukio](https://kitoto.files.wordpress.com/2019/07/1-bango-la-tukio.jpg)
![6- Mavazi ya All Things African - pic by F Macha, 2019.jpg](https://kitoto.files.wordpress.com/2019/07/6-mavazi-ya-all-things-african-pic-by-f-macha-2019.jpg)
Bidhaa mbalimbali za Kitanzania zilizooneshwa na Wajasiriamali
![16- Wajisiramali- Laila Hamza, Noeta, Anna Lukindo na Sia Travel- pic by F Macha 2019.jpg](https://kitoto.files.wordpress.com/2019/07/16-wajisiramali-laila-hamza-noeta-anna-lukindo-na-sia-travel-pic-by-f-macha-2019.jpg)
Toka kushoto. Wajasiria mali, Laila Hamza, Noeta, Anna Lukindo ( mwendeshaji wa mitindo ya "Anna Luks") na Sia Travel (Biashara ya utalii na mwalimu wa Kiswahili )
![18- Washiriki wakiwa na Patronella Mlowe (pili toka kushoto- pic by F Macha, 2019.jpg](https://kitoto.files.wordpress.com/2019/07/18-washiriki-wakiwa-na-patronella-mlowe-pili-toka-kushoto-pic-by-f-macha-2019.jpg)
![19-Mavazi yaliyooneshwa- pic by F macha 2019](https://kitoto.files.wordpress.com/2019/07/19-mavazi-yaliyooneshwa-pic-by-f-macha-2019.jpg)
Baadhi ya mavazi mengi ya Kitanzania, yaliyooneshwa
Post a Comment