MTANGAZAJI

MKUU WA WILAYA AWATAKA WANAWAUME KUWAPA WANAWAKE HAKI YA KUMILIKI ARDHI

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa na viongozi mbalimbali akiwa kwenye banda la mradi wa urasimishaji ardhi vijiji (LTA) ambao ndio wamesaidia kutoa hati miliki kwa wanawake na kupunguza migogoro wilaya ya Iringa
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka wanaume kuwapa haki wanawake ya kumiliki ardhi kwa kuwa wanahaki hiyo kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi hivyo mwanaume atakayemkataza mwanamke kumiliki ardhi atachukuliwa hatua za kisheria.
 
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Iringa Richard Kasesela katika kilele cha maadhimisho ya wanawake yaliyofanyika katika kijiji cha Ibangamoyo kata ya Ulanda wilaya ya Iringa alisema kuwa wanawake waaze kumiliki ardhi ili kujiinua kiuchumi kwa kuwa wanawake ndio walezi wa familia tofauti na wanaume wanaokuwa na makazi tofauti tofauti.

 
Amesisitiza kuwa Wanawake  mkoani humo  wanapaswa kumiliki ardhi kwa ajili ya kufanya shughuli za kimaendeleo na badala yake waachane na tamaduni kandamizi za kuwaachia wanaume katika umiliki wa mali.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.