MTANGAZAJI

JENGO KUBWA KABISA DUNIANI AMBALO NI KARAKANA YA KUUNGANISHA NDEGE ZA BOEING (+VIDEO)



 

Jengo kubwa kabisa duniani (sio refu, bali kubwa) ni karakana ya kuunganisha ndege za Boeing  747, 767, 777, na  787  liko  Washington State nchini Marekani.

 Jengo hili lina ukubwa wa futi za mraba zaidi ya milioni 472. 

Jengo hili ni kubwa kiasi kwamba kabla halijawekewa mfumo maalum wa kuzungusha hewa, lilikuwa likitengeneza mawingu ndani ya jengo. 

Ni hapa ambapo ndege za Boeing zimekuwa zikiunganishwa tangu enzi za vita ya pili ya dunia. 

Baadhi ya mambo muhimu kujua ni.... 

1: Jengo hili liko kwenye eneo la ekari 98.7, lina wafanyakazi 30,000 ambamo humo ni kama jiji. Kuna migahawa dazeni kadhaa. Huduma za kulea watoto (child care), ATMs na kadhalika. 

2: Lina njia za chini ya ardhi kwa watembea kwa miguu zenye urefu wa maili 2.33 kuwawezesha wafanyakazi 'kusafiri' toka upande mmoja wa jengo hadi mwingine. 

3: Lina zaidi ya taa milioni moja. 

4: Lina zaidi ya baiskeli na guta 1,300 kuwawezesha wafanyakazi kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine

Na Mubelwa Bandio.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.