MTANGAZAJI

CHAVITA YAIOMBA SERIKALI YA TANZANIA KUWAWEZESHA KWA KUWAPATIA MIKOPO YA FEDHA


Mmoja wa washiriki akielezea changamoto za watu wenye ulemavu wa kusikia  kwa kutumia lugha ya alama, likiwemo suala la mawasiliano,  katika Semina ya Elimu ya Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha kwa makundi maalum iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango, mkoani Mwanza.
Baadhi ya washiriki wa Semina ya Elimu ya Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha kwa makundi maalum wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango , Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye ulemavu wa kusikia mkoani Mwanza (CHAVITA) Jones George, ameiomba Serikali kuweka mazingira wezeshi kwa wenye ulemavu wa kusikia  kupata mikopo ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Ombi la Jones Goerge amelitoa kwenye wa  mafunzo ya elimu ya Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha kwa watu wenye ulemavu wa kusikia  kwa lengo la kuwajengea uwezo na kushirikishwa katika Huduma Jumuishi za Fedha yanayoendeshwa  na Wizara ya Fedha na Mipango nchini Tanzania yanayofanyika mkoani Mwanza.


Akizungumza katika mafunzo hayo, Mchumi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dionisia Mjema, ameeleza kuwa mafunzo hayo yameanza mkoani Mwanza na yanatarajia kuwafikia makundi maalumu yote na wananchi wa hali ya chini ili  kuwawezesha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya kuinua maisha yao na kuchangia katika uchumi wa nchi.

Katibu Mtendaji wa Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Maendeleo ya watu wenye ulemavu wa kusikia Tanzania   (TAMAVITA), Kelvin Nyema, ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuandaa mafuzo hayo ambapo ameeleza kuwa 
tatizo kubwa linaoowakabili ni mawasiliano ambayo yanasababisha wasishirikishwe katika shughuli mbalimbali za maendeleo na za kijamii. 

Alisema hali ya watu wenye ulemavu wa kusikia ni ngumu, hawana elimu yoyote ya masuala ya fedha na hawajui waanzie wapi huku akibainisha kuwa kuna wakati wanaogopa kukopa kwa dhana kuwa wakikopa watafungwa.


Akizungumza katika mafunzo hayo, Mchumi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dionisia Mjema, ameeleza kuwa mafunzo hayo yameanza mkoani Mwanza na yanatarajia kuwafikia makundi maalumu yote na wananchi wa hali ya chini ili  kuwawezesha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya kuinua maisha yao na kuchangia katika uchumi wa nchi.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.