NCHI ZILIZOENDELEA KITEKNOLOJIA ZISAIDIE KUBORESHA HARAKATI ZA UCHUMI WA VIWANDA-SAMIA
Nchini
zilizopiga hatua katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia zimetakiwa
kuwa tayari kusaidia kuleta teknolojia hiyo ili kukabiliana na athari
zinazoweza kujitokeza za kimazingira katika harakati za kufikia
maendeleo ya uchumi wa viwanda.
Akizungumza
kwenye maadhimisho ya 72 ya Umoja wa Mataifa (UN) na wageni waalikwa
kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia
Suluhu Hassani amesema kwamba maendeleo ya viwanda yanakwenda sambamba
na tishio la uharibifu wa mazingira na tabianchini ni muhimu kwa wadau
wote wa maendeleo kujipanga.
Amesema
nchini juhudi zinaendelea za kukuza uchumi na maendeleo ya watu lakini
ni muhimu kwa wananchi kwa ujumla wao kuweza kulinda na kuhifadhi zaidi
maliasili, hifadhi na rasilimali za taifa ili kuweza kufikia uchumi wa
viwanda.- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez mara baada ya kuwasili kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Aliongeza
kwamba ofisi yake ambayo inashughulikia mambo ya tabianchini na
mazingira wametunga sera, sheria na sera mpya ya mazingira na uendeshaji
wa mambo ya mazingira pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2016 ambapo
ni kuhakikisha juhudi za viwanda haziwezi kuathiri mazingira ya nchini
Amesema
kwamba ni takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwa agenda za
maendeleo endelevu 2030, ambapo malengo 17 yamewekwa na Tanzania
imefanikiwa kuingia kwenye awamu ya pili ya maendeleo endelevu katika
juhudi za kupambana na umasikini
- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki na Afisa Mwakilishi wa Unesco Dar, Ann Therese Ndong- Jatta mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee kushiriki maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
sss
- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga pamoja na 10) Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez wakishuhudia bendera ya Umoja wa Mataifa ikipandishwa kuashiria kilele cha maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
- Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga akiazungumza machache kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) kuzungumza kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akihutubia hadhara ya wageni mbalimbali (hawapo pichani) na kusisitiza umuhimu wa teknolojia katika kufikia uchumi wa viwanda wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
- Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan ya heshima kwa kutambua ushirikiano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Post a Comment