MTANGAZAJI

NCHI ZILIZOENDELEA KITEKNOLOJIA ZISAIDIE KUBORESHA HARAKATI ZA UCHUMI WA VIWANDA-SAMIA


Nchini zilizopiga hatua katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia zimetakiwa kuwa tayari kusaidia kuleta teknolojia hiyo ili kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza za kimazingira katika harakati za kufikia maendeleo ya  uchumi wa viwanda.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya 72 ya Umoja wa Mataifa (UN) na wageni waalikwa kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani amesema kwamba maendeleo ya viwanda yanakwenda sambamba na tishio la uharibifu wa mazingira na tabianchini ni muhimu kwa wadau wote wa maendeleo kujipanga.
Amesema nchini juhudi zinaendelea za kukuza uchumi na maendeleo ya watu lakini ni muhimu kwa wananchi kwa ujumla wao kuweza kulinda na kuhifadhi zaidi maliasili, hifadhi na rasilimali za taifa ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez mara baada ya kuwasili kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Aliongeza kwamba ofisi yake ambayo inashughulikia mambo ya tabianchini na mazingira wametunga sera, sheria na sera mpya ya mazingira na uendeshaji wa mambo ya mazingira pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2016 ambapo ni kuhakikisha juhudi za viwanda haziwezi kuathiri mazingira ya nchini
Amesema kwamba ni takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwa agenda za maendeleo endelevu 2030, ambapo malengo 17 yamewekwa na Tanzania imefanikiwa kuingia kwenye awamu ya pili ya maendeleo endelevu katika juhudi za kupambana na umasikini
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki na Afisa Mwakilishi wa Unesco Dar, Ann Therese Ndong- Jatta mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee kushiriki maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwakilishi wa UNFPA nchini, Jacqueline Mahon mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwakilishi wa UNICEF nchini, Maniza Zaman mara baada ya kuwasili katika maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
sss
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akipokea heshima katika maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride la heshima katika maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga pamoja na 10) Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez wakishuhudia bendera ya Umoja wa Mataifa ikipandishwa kuashiria kilele cha maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga  akiazungumza machache kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) kuzungumza kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akihutubia hadhara ya wageni mbalimbali (hawapo pichani) na kusisitiza umuhimu wa teknolojia katika kufikia uchumi wa viwanda wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa huo yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan ya heshima kwa kutambua ushirikiano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo ya heshima Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Pichani juu na chini ni baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, viongozi wa Serikali pamoja na wadau wa maendeleo waliohudhuria sherehe za miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Weruweru wakitoa burudani kwa vitendo kwenye maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na wakuu wa mashirika yaliyochini ya Umoja wa Mataifa nchini wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja huo.
Mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania
Mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja wanafunzi wa shule ya Sekondari Dodoma, Weruweru na Zanzibar.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje katika picha ya pamoja.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiagana na baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.