MTANGAZAJI

KAMPALA:MWIMBAJI WA THE LIVING VOICES AZIKWA KIJIJINI KWAO






Mjane (aliyekuwa Mke wa Marehemu Nyombi Steven katikati) akiwa na Mwalimu wa The Living Voices Enock Kawaase kushoto wakiwa na Mwimbaji wa Blessed Hamony ,Fadhili toka Tanzania wakati wa mazishi hii leo.
Waimbaji wa The Living Voices wakiwa na Mwimbaji toka Tanzania Fadhili huko Kayunga kwenye shughuri ya Mazishi ya Nyombi Steven

Nyombi Steven wakati wa uhai wake
Mamia ya Waumini wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato na Madhehebu mengine Oktoba 7 mwaka huu wameshiriki  katika maziko ya Mwimbaji Mahiri wa Sauti ya Tatu wa kwaya ya nyimbo za Injili The Living Voices ya nchini Uganda Nyombi  Steven aliyefariki juzi usiku baada ya kugongwa na gari wakati akielekea nyumbani baada ya kutoka Kazini.


Nyombi amezikwa  kijiji kijijini kwao Kayunga umbali wa mile 45 toka  jiji la Kampala Uganda huku tukio hilo likishuhudia zaidi ya kwaya 10 za madhehebu tofauti tofauti zilizoimba usiku kucha

 

Marehemu Nyombi aliyezaliwa miaka 45 iliyopita   alianza kuimba na Kwaya ya Jerusalem Pipers na alikuwa ni Miongoni mwa waimbaji waanzilishi wa The Living Voices ambayo nyimbo zao husikika kupitia Morning Star Radio na Morning Star TV alililelewa Shangazi yake ambaye ni mwimbaji na analala mauti akiwa amedumu katika kwaya hiyo kwa muda wa miaka 16 na ameacha mjane na watoto sita,wakike wanne na wakiume wa wawili.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.