MTANGAZAJI

DC MTATURU AAGIZA WATAALAMU WA KILIMO KUWAUNGANISHA WAKULIMA NA MFUMO WA BENKI YA KILIMO

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumzia katika kikao Cha kazi na wataalamu wa Kilimo, Ufugaji na Mipango miji.
Wataalamu wa Kilimo, Mifugo na Mipango Miji katika Halmashauri ya Itigi na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni wakimsikiliza kwa makini Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati wa kikao Cha kazicha namna ya kuboresha kilimo, Ufugaji na Mipango Miji.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumzia katika kikao Cha kazi na wataalamu wa Kilimo, Ufugaji na Mipango miji.
Wataalamu wa Kilimo, Mifugo na Mipango Miji katika Halmashauri ya Itigi na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni wakimsikiliza kwa makini Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati wa kikao Cha kazicha namna ya kuboresha kilimo, Ufugaji na Mipango Miji.


Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumzia katika kikao Cha kazi na wataalamu wa Kilimo, Ufugaji na Mipango miji.


Wataalamu wa Kilimo wametakiwa kuwaunganisha wakulima na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa ajili ya kusaidia upatikanaji wa Masoko ili kuongeza Mapinduzi yenye tija katika Sekta ya Kilimo.

Akizungumzia katika kikao Cha kazi na wataalamu wa Kilimo, Ufugaji na Mipango miji Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa pamoja na wananchi kujituma katika uzalishaji wa mazao ya chakula na kilimo lakini changamoto Ni kubwa ya namna ya kuongeza ufanisi katika masoko.

Alisema kuwa endapo wakulima wataunganishwa na Benki ya Kilimo itakuwa Ni njia pekee ya kuchagiza na kusaidia kuwezesha Sekta ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda kilimo cha kibiashara ili kukuza uchumi na kupunguza umasikini.

Alisema kuwa Katika kutekeleza majukumu ya wananchi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania imeanza huduma zake kwa kulenga minyororo michache ya ongezeko la thamani katika kilimo ambapo mikopo ya aina mbalimbali hutolewa kuwezesha wakulima kuongeza tija na uzalishaji katika sekta ya kilimo nchini Tanzania. 

Katika kikao hicho Cha kuwakumbusha majukumu wataalamu hao Mhe Mtaturu amewataka kuandaa mpango kazi wa mazao ya Kilimo hususani mazao ya chakula na Biashara.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.