MTANGAZAJI

WAZIRI WA FEDHA WA TANZANIA AKAGUA NA KUTOA MAAGIZO KUHUSU MADINI YA ALMASI YALIYOKAMATWA



 

Sehemu ya Mzigo  wa Almasi uliokamatwa katika uwanja wa Ndege ambao thamani yake ni zaidi ya Tsh. Bilioni 64.


Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Filip Mpango akisoma maelezo ya mzigo huo ambayo yalikuwa tofauti kabisa na uhalisia mara baada ya kuhakikiwa na timu ya  Wataalamu wa Kitanzania wazalendo.




Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania  Dkt. Philip Isdor Mpango ameviagiza vyombo vinavyohusika kuchukua hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Williamson Diamond Ltd na wote waliohusika kuidhinisha usafirishaji wa madini ya almasi kutoka migodi ya kampuni hiyo na kudanganya thamani halisi ya madini hayo kwa lengo la kuisababishia hasara Serikali. 


Dkt. Mpango ametoa agizo hilo leo septemba 09 baada ya kukagua madini ya almasi yaliyokamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam yakisafirishwa kupelekwa nchini Ubelgiji.



Miongoni mwa hatua za kisheria zitakazo chukuliwa na serikali ya Tanzania ni pamoja na kutaifisha madini yote ya almasi yaliyokamatwa baada ya kubainika udanganyifu wa thamani yake halisi.


Almasi hiyo ilikamatwa Agosti 31 mwaka huu muda mfupi kabla ya kupakizwa kwenye ndege ili isafirishwe kwenda nchini Ubelgiji, na ilipochunguzwa ilibainika kuwa nyaraka za kampuni ya Williamson Diamond Ltd zimeonesha kuwa almasi hiyo ina thamani ya Dola za Marekani Milioni 14.798 sawa na Shilingi Bilioni 33 za Tanzania wakati thamani yake halisi ni Dola za Marekani Milioni 29.5 sawa na Shilingi Bilioni 65 za Tanzania.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.