ZANZIBAR:UN, SMZ KUSHIRIKIANA KUKOMESHA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa
habari katika ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto, Mkoa wa Kaskazini
Unguja katika Kijiji cha Mahonda wakati wa ziara fupi ya kukagua miradi
inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa visiwani humo ikiwa ni sehemu ya
maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja huo tangu kuanzishwa.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez amesema Umoja huo utaendelea
kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) katika kukomesha
vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.
Akizungumza
katika ziara ya kutembelea Dawati la jinsia la Wanawake na Watoto, Mkoa
wa Kaskazini Unguja katika Kijiji cha Mahonda alisema umoja huo
umelenga kusaidia uwepo wa utawala wa sheria na wenye kujali haki na utu
wa binadamu kupitia mpango mkakati wake uliomo katika malengo ya
maendeleo endelevu (SDGs) kuanzia mwaka 2016 utakosaidia kuondoa vitendo
hivyo.
Alieleza
kuwa tatizo la udhalilishaji wa kijinsia sio kwa Zanzibar pekee bali
ni la kidunia, hivyo umoja wa mataifa(UN) unawajibu kusaidia juhudi za
serikali kupambana na tatizo hilo.
Mtendaji
wa Dawati la Jinsia na Watoto, Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Kijiji
cha Mahonda, kutoka Jeshi la Polisi Koplo, Fatma Juma akitoa taarifa
fupi ya maendeleo ya kituo hicho tangu kufunguliwa ikiwa ni mwaka mmoja
sasa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi
wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (hayupo pichani)
ikiwa ni awamu yake ya pili kutembelea Dawati hilo. Kulia ni Mtaalamu
wa masuala ya ulinzi kwa watoto wa UNICEF Zanzibar, Bw. Ahmed Ali.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akipitia kitabu cha orodha za
kesi katika Dawati la Jinsia na Watoto, Mkoa wa Kaskazini Unguja katika
Kijiji cha Mahonda. Kulia ni Mtendaji wa Dawati hilo, kutoka Jeshi la
Polisi Koplo, Fatma Juma na kushoto ni Mtaalamu wa masuala ya ulinzi
kwa watoto wa UNICEF Zanzibar, Bw. Ahmed Ali.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiwa ndani ya chumba cha
dawati la Jinsia.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiagana na Mkuu wa Upelelezi
wa Dawati la Jinsia na Watoto, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Kombo Khamis
Kombo (kulia) alipofanya ziara ya kutembelea Dawati la Jinsia na Watoto,
Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Kijiji cha Mahonda ikiwa ni sehemu ya
maadhimisho ya sherehe za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa tangu
kuanzishwa. Kushoto ni Mtaalamu wa masuala ya ulinzi kwa watoto wa
UNICEF Zanzibar, Bw. Ahmed Ali.
Mradi huu ulifadhiliwa kwa pamoja kati ya Jumuiya ya Ulaya (EU) na Shirika linalohudumia watoto duniani, UNICEF.
Muonekano wa jengo la Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Kaskazini Unguja.

Post a Comment