MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:MAMLAKA YA HALI YA HEWA NCHINI TANZANIA YAELEZA HALI YA MVUA OKTOBA MPAKA DESEMBA 2015




Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya hali ya hewa Tanzani   Agness Kijazi
Mamlaka ya hali ya hewa nchini Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya tathimini ya mvua za masika na mvua za vuli kwa muda kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2015.


Mkurugenzi wa  mamlaka ya hali ya  hewa  Dkt Agnes kijazi  amesema Msimu wa mvua wa miezi ya Oktoba hadi Disemba (vuli) ni mahususi katika maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki (Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara), pwani ya kaskazini (Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro-kaskazini pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba), kanda ya Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza, Geita, Simiyu na Shinyanga) na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma.


Mvua za Oktoba-Novemba-Disemba 2015, zinatarajiwa kuwa za juu ya wastani na wastani katika maeneo mengi yanayopata misimu miwili ya mvua. 

Maeneo machache ya kusini mwa nchi yanatarajiwa kupata mvua za chini ya wastani.


Msikilize Mkurugenzi  Mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa  Agnes Kijazi anaeleza hapa

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.