MTANGAZAJI

MAMBO 15 KUHUSU MABASI YAENDAYO HARAKA DART.



 

Huenda umeshayaona ama kupanda mabasi yaendayo haraka ya Dart jijini Dar es salaam yafuatayo ni mambo 15 unayopaswa kuyafahamu kuhusu mabasi hayo  

1. Kiwanda Kilicho Assemble (Kuunganisha) Mabasi haya kinaitwa Golden Dragon cha China.

2. Aina ya Injini ni CUMMINS ya Marekani (USA)

3. Aina ya Giaboksi ni VOITH ya Ujerumani.

4. Mfumo wa Stelingi ni ZF ya Ujerumani.

5. Mgumo wa Difu ni kutoka Marekani (USA).

6. Aina ya Suspension (Za upepo) Air Suspension kutoka Marekani (USA).

7. Mfumo wa Breki ni WABCO


8. Aina za Mabasi ziko mbili. Articulated Mita kumi na nane almaarufu (Ikarusi) Kutoka Hungary zitakazopita kwenye barabara Maalumu za zege zilizojengwa na Mabaai ya mita kumi na mbili yanayoitwa (Feeder) Mabasi Mlisho yatakayotumia vituo vilivyoko nje ya mfumo Mfano Kituo cha Shekilango, Moroco Hotel, Mwanamboka na Magomeni Mapipa kuwapeleka na kuwaleta kwenye Mfumo.

9. Milango ya kupanda na kushukia Abiria ipo kulia na kushoto ili kukidhi mahitaji ndani na nje ya mfumo ambayo idadi yake ni Minne kila upande ila itatumika mitatu na mmoja niwa dharula kila upande.


10. Urefu kutoka ardhini kwa milango ya kushoto ya Basi ni Sentimita thelathini (30) ambayo hata mtoto anaweza kushuka bila msaada wa mtu mzima.

11. Urefu wa Milango ya kulia ni Sentimita tisini (90) sawa na urefu wa Platform za kila kituo cha DART unaomuwezesha hata mtu mwenye mahitaji maalum Kuingia na kutoka ndani ya basi bila msaada wa mtu.

12. Ndani ya basi kuna eneo la kukaa watu wenye Mahitaji maalum.
Walemavu, Wazee na Mama wajawazito.


13. Mfumo wa ulipaji nauli unafanyika vituoni kama ilivyo kwenye kivuko pale Kivukoni hivyo basi hili halina Kondokta. Makondakta wapo vituoni.

14. Muda wa Safari kutoka Kivukoni hadi kimara ni wastani wa dakika thelathini (30) ikihusisha muda wa kushusha na kupakia kwenye Vituo vya DART.

15. Ni marufuku kwa chombo ama mwananchi kutumia barabara maalum za Mabasi. Wananchi watumie maeneo yaliyotengwa maalum kulingana na mahitaji. 

Watumiaji wa Bodaboda wanatakiwa kupita kwenye barabara zinazotumiwa na magari ya Kawaida na siyo eneo lililotengwa kwa ajili ya Watembea kwa Miguu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.