MTANGAZAJI

KIGOMA:WATU WASIOFAHAMIKA WATEKETEZA NYUMBA 8 KWA SIKU MBILI



 Nyumba nane katika kijiji cha Kazilamihunda kata ya Kasanda wilayani Kakonko mkoani Kigoma zimeteketezwa kwa moto na watu wasiofahamika katika kipindi cha siku mbili mfululizo.

 Mtendaji wa kijiji hicho Bw.Heziloni Mayunga amesema matukio hayo yametokea usiku wa kuamkia jumatatu na kuamkia jumanne na kusababisha baadhi ya wananchi kukimbia makazi yao na kulala porini wakihofia maisha yao.

Bw.Mayunga amesema kuwa usiku wa kuamkia jana nyumba nne ziliteketezwa kwa moto na kusababisha hasara kubwa kwa wakazi hao ikiwemo kuungua kwa mazao na mavazi.

Mmoja wa wahanga wa tukio hilo Bw.Rauliani Wilbadi amesema kuwa kwa sasa wanapata wakati mgumu ambapo hulazimika kulala nje, hali ambayo inahatarisha usalama wao.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.