MTANGAZAJI

TANZANIA YAENDELEA KUAGIZA SUKARI TOKA NCHI ZA NJE






Serikali ya Tanzania inalazimika kuagiza tani 290,000 za sukari kila mwaka toka nchi za nje ili kufidia pengo la uzalishaji wa sukari nchini humo.

Kwa mujibu wa  Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika nchini Tanzania  Godfrey Zambi, ambapo anaeleza kuwa  mahitaji ya sukari nchini humo  kwa mwaka ni wastani wa tani 590,000 huku tani 420,000 zikiwa ni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na tani 170,000 za viwandani.

Taarifa ya waziri huyo inaonesha kuwa  uzalishaji wa sukari nchini Tanzania kwa mwaka ni wastani wa tani 300,000 ambazo ni kwa matumizi ya nyumbani tu ambapo, msimu wa mwaka 2014/15, serikali iliidhinisha tani 100,000 tu za sukari ya matumizi ya kawaida kuingizwa nchini humo kati ya Machi na Mei mwaka huu.

Tani 182,765 ziliidhinishwa kuingizwa nchini kati ya Julai 2014 na Juni 2015 kwa ajili ya matumizi ya viwandani.

Naibu Waziri huyo amesema punguzo la ushuru kwa sukari inayoingizwa nchini pamoja na kusaidia bei ya sukari kupungua, imekuwa ikisaidia bei ya mlaji kutopanda.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.