MTANGAZAJI

MAKAMU WA MWENYEKITI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO DUNIANI AWATAKA WAUMINI NCHINI KUDUMISHA MAHUSIOANO MEMA

Makamu wa Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani Mch Geofrey Gabriel Mbwana akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kanisa hilo Kanda ya Mashariki mwa Tanzania Mch Mark Walwa Malekana


Mch Geofrey Gabriel Mbwana akihutubia

Mch Mark Walwa Malekana akisalimu waumini

Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Lugalo

Waimbaji wa Mwananyamala SDA Choir



Waimbaji wa Mbezi Beach SDA Choir

Waimbaji wa Kwaya ya KKKT Usharika wa Salasala wakifuatilia

Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la RC la Mbezi Beach



Makamu wa mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani Mchungaji Geofrey Gabriel Mbwana amewataka waumini wa madhehebu mbalimbali nchini kudumisha mahusiano mema japokuwa wanamitazamo tofauti katika masuala ya imani.


Akihutubia hii leo kwenye sabato maalum ya ujirani mwema na uimbaji  iliyofanyika kwenye kanisa la Waadventista Wa Sabato Mbezi Beach jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na waumini wa madhehebu mbalimbali Mchungaji Mbwana amesema kuna haja ya waumini hao kuyatazama zaidi masuala ya imani wanayofana na kuyajadili kwa upendo na amani yale wanayotofautiana.


Naye Mwenyekiti wa Konferensi ya Mashariki mwa Tanzania (ETC) ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Mchungaji Mark Walwa Malekana akimshukuru Kiongozi huyo kwa ukubali wake kushiriki kwenye ibada hiyo amesema pamoja na watanzania kutoka katika madhehebu mbalimbali hapa nchini basi wanapaswa kutokuwa na chuki kutokana na tofauti za kiimani.


Ibada hiyo ambayo ilirushwa moja kwa moja na Morning Star Radio katika kipindi cha Ibada makanisani pia ilihudhuriwa na Waimbaji wa Kwaya ya KKKT Usharika wa Salasala,Kwaya ya Kanisa la RC la Mbezi Beach na Kwaya za Makanisa ya Waadventista Wa Sabato Lugalo,Mbezi Beach na Mwananyamala.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.