MTANGAZAJI

MARA:MAKAMPUNI YACHANGIA UJENZI WA MABWENI YA SHULE YA NYASINCHA YALIYOUNGUA MWEZI SEPTEMBA

Mgodi wa dhahabu wa African Barrick Gold North Mara kwa ushirikiano na kampuni saba wametoa msaada wa zaidi ya shilingi  23 milioni kusaidia ujenzi wa vyumba vitatu vya mabweni ya wavulana katika Shule ya Sekondari Nyansincha vilivyoungua moto Septemba 15 mwaka huu.

Katika msaada huo mgodi huo umetoa shilingi  13 milioni, kampuni ya Mara kaskazini  bati 30, duka la vifaa vya ujenzi Chakechake mifuko 20 ya saruji yenye thamani ya shilingi 800,000,  kampuni ya AKO vitanda  26 vya deka, Kundi la Kemambo shilingi 200,000, Gimunta Champion shilingi milioni moja, Borrtech (T) ltd shilingi 3 milioni na kampuni ya Magnet ilitoa shilingi 1.5 milioni.

Akikabidhi msaada huo kwa shule hiyo inayomilikiwa na Kanisa la Waadventista Wa Sabato Meneja wa mgodi wa ABG North Mara, Garry Chapman amesema, kupatikana kwa msaada huo kutoka kwa wadau ni umoja na ushirikiano walionao katika kazi huku wakionyesha kuguswa na tukio la mabweni  matatu kuteketea na kuwafanya wanafunzi kupata shida ya masomo.

Akipokea msaada huo Mkuu wa shule hiyo Japhet Mugini alisema msaada huo utawasaidia kufikia katika hatua nzuri ambayo itawafanya wanafunzi waanze kulala katika vitanda vyao wenyewe tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo wanalala wawili wawili kenye kitanda kimoja.

Mabweni matatu ya wavulana  ya Shule ya Sekondari ya Nyansicha yalichomwa moto septemba 15 majira ya saa 11 jioni na mwanafunzi wa kidato cha pili Michael Kimunye aliyedhaniwa kuwa na ugonjwa wa mapepo ambapo moto huo uliteketeza mali ya wanafunzi na shule yenye thamani ya sh, 113.6 milioni.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.