MTANGAZAJI

KIONGOZI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO AWATAKA WATU KUMWEKA MUNGU MBELE


Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato  katika Konferensi ya Mara Mchungaji Daudi Makoye amewataka watu kuyashika maneno ya Mungu ili waweze kufanikiwa katika maisha yao.
Kiongozi huyo ametoa agizo hilo mwishoni mwa juma jijini Mwanza wakati akihutubia kwenye kilele cha mkutano wa Mkutano wa Chama cha Wanataaluma na wajasiriamali Waadventista  Wa Sabato Tanzania  (ATAPE) uliokuwa ukifanyika kwenye hoteli ya JB Belmonte jijini humo ambao pia uliwahusisha watu wenye ulemavu wa ngozi albino.
Katika mkutano huo ambapo kulifanyika  ibada  ya kuwaombea watu wenye ulemavu  wa ngozi albino na taifa la Tanzania Mchungaji Makoye amesema jamii inatakiwa kuonyesha juhudi ya kumweka Mungu mbele ili awe ngao na kinga katika maisha.
Amesema mtu yeyote asitegemee akili ya mtu mwingine ili aweze kufanikiwa bali kila mmoja afanye kwa uwezo na akili yake mwenyewe binafsi aliyopewa na Mungu na siyo kutegemea utajiri kutoka kwa viungo vya albino.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa ibada hiyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Arusha Dr  Moses Muneja amewataka watu wote kuwa na moyo wa huruma na kujitolea kutoa misaada yao inapohitajika bila kujali kupata malipo.
Mkutano huo ambao ulikuwa wa kwanza kuwahusisha watu wa rika na kada mbalimbali  ulihudhuriwa na Mwakilishi wa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Sheikh Abdalah Hija na Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato wa Unioni ya Kaskazini Mwa Tanzania Dr Godwin Lekundayo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.