MTANGAZAJI

VIONGOZI WA KANISA WAOMBA WAUMINI KUSHIRIKI KATIKA SIKU YA AMANI DUNIANI-SEPTEMBA 21,MWAKA HUU

-->
Adventist Church to mark UN’s International Day of Peace September 21
Viongozi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Duniani wamewataka waumini wa Kanisa hilo kuungana na kushiriki katika siku ya amani itakayoadhimishwa na umoja wa Mataifa Septemba 21 mwaka huu  kwa kufanya maombi ya mchana katika muda wa dakika moja ya ukimya iliyopangwa kwa siku hiyo.

Wito huo umetolewa kufuatia taarifa ya maandalizi iliyotolewa na Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon inayowataka watu kuakisi amani na kuongeza kuwa ni lazima kila mtu kupingana na sababu zozote zinazoweza kuleta mapigano na kuelezea kuwa amani ndiyo njia watu wote wanayopaswa kusafiri kwayo hatua kwa hatua.

Taarifa iliyotolewa  na Kanisa la Waadventista wa Sabato kupitia kwa mkurugenzi wa idara ya uhusiano  na uhuru wa dini John Graz imesema waumini wa Kanisa hilo wanapaswa kuwa  na amani na watu wote,na kuweka bayana kuwa Yesu Kristo mwenyewe anawataka wafuasi wake kuwa watu wa amani ndani ya jamii na kuwa mkono wa mbaraka kwa watu wengine.

Graz amesema ili kuboresha amani Duniani Kanisa linapaswa kuwekeza katika maendeleo ya Elimu,Afya,haki na uhuru kwa watu wote ndiyo maana kama kanisa hilo lina Shule,Hospital na taasisi mbalimbali za kusaidia raia.
Chanzo:ANN

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.