MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WASHIRIKI WA KANISA WATAKIWA KUTOISHI MIJINI BILA KAZI



Katibu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Unioni Misheni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji James Machage amewataka  washiriki wa kanisa hilo wanaoishi mijini bila kufanya kazi  kurudi vijijini  na kujihusisha na kazi za kilimo ili kuleta maendeleo ya kanisa na  jamii kwa ujumla.

Mchungaji Machage ametoa agizo hilo katika kanisa la Waadventista Wa Sabato  Magomeni anapoendesha mkutano wa juma la uamusho la uwakili lililoanza sabato iliyopita ambapo amesema inashangaza watu wengi kuishi katika maeneo ya miji mikubwa kama Dar es salaam na hawana kazi za kufanya hali inayofanya waongeze msongamano wa watu  wakati kuna maeneo makubwa vijijini yanayohitaji kuendelezwa.

Machage amesema kuwa serikali haina uwezo wa kuwapatia watu wote ajira hivyo inapaswa wananchi watumie elimu waliyonayo kukabiliana na mazingira na kujipatia maendeleo yao wenyewe huku akisisitiza kuwa miji yenye msongamano wa watu kama Dar es salaam waishi watu walio na kazi tayari.

Mchungaji Machage ambaye kitaaluma ni mtaalamu wa masuala ya anga amesema imefika wakati sasa kwa waumini wa kanisa kuweka juhudi katika kutumia elimu waliyonayo kufanyakazi kwa bidii na kujipatia maendeleo binasfi na kusaidia miradi mbalimbali ya kanisa na kama mtu anaelimu na hana kazi ya kufanya ni vema kuchukua maamuzi ya kwenda kijijini kulima na si kuishi mjini wakati hana jambo la kufanya.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.