MTANGAZAJI

PWANI:MWONGOZO WA VIWANGO VYA WADAU WA HABARI NA UJUMBE SAHIHI KUHUSU UKIMWI (VVU) WATOLEWA



Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP) hivi karibuni  umezindua mwongozo wa Taifa wa Kupitia na Kuhakiki nyenzo za habari, elimu na mawasiliano ya kubadili tabia kwa lengo la kuboresha habari na mawasiliano yanayofanywa  na Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii na wadau wake kwa lengo la kuthibiti kuenea kwavirusi vya UKIMWI (VVU).

NACP  iliyopo chini ya Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii ikiwa na jukumu la kusimamia masuala yakinga, tiba, matunzo na misaada kwenye nyanja ya UKIMWI ka tika sekta ya afya nchini, imezindua mwongozo huo kwa wadau wa habari, elimu na mawasiliano (IEC) na mawasiliano ya Kubadili Tabia (BCC), mjini Bagamoyo.

Mwongozo huo wa kwanza kwenye sekta ya afya unalenga kuweka viwango vya kitaifa kwa wadau wa mawasiliano ambapo nyenzo zote za machapisho na za kielektroniki za IEC/BCC zitapaswa kuhakikiwa na idara hiyo kwa lengo la kuboresha ujumbe unaotolewa.

Lengo kubwa la mwongozo huo huo ni kuhakikisha matangazo yote yanayohusu kinga, tiba, matunzo na misaada kwenye nyanja ya UKIMWI yana hakikiwa ubora ili kutoa ujumbe sahihi kwa walengwa katika jitihada za serikali za kuunga mkono jitihada za wadau wanaojihusisha na afua za ugonjwa huo.

Katika dibaji ya mwongozo huo, Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Donan Mmbando anasema licha ya juhudi kubwa ya uenezaji na upatikanaji wa shughuli za habari na mawasiliano kuhusu VVU na UKIMWI nchini,bado kuna baadhi ya ujumbe usiostahili  unaotolewa kwa walengwa.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.