MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:BOT KUTOA KUZINDUA SARAFU YA SHILINGI 500



Benki kuu ya Tanzania (BOT),inatarajia kuzindua sarafu ya shilingi 500 itakayochukua nafasi ya shilling mia tano ya noti.

Akizungumza hapo jana katika banda la BOT kwenye viwanja vya maonesho ya kimataifa ya biashara ya 38 ya sabasaba jijini Der es salaam,afisa mwandamizi wa benk hiyo,Hawa Muro,amesema kuwa wamefikia hatua hiyo kutokana na kuwapo kwa utunzaji mbovu wa noti ya shilingi 500.

Muro amesema kuwa katika uchunguzi uliofanywa wamegundua kuwa wananchi wengi wanashindwa kuitunza noti hiyo kutokana na mzunguko mrefu iliyonayo kwa watumiaji.

Amesema BOT,inaamani kuwa sarafu ya shilingi 500 ndiyo itakayo dumu kwa muda mrefu katika mzunguko wa pesa nchini.

Muro amesema  mchakato wa mabadiliko hayo ambao unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha mwaka wa 2014/2015 ambapo sarafu hiyo itazinduliwa na benki hiyo ili wananchi waanze kuitumia.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.