MTANGAZAJI

WAZIRI MKUU AITAKA WIZARA KUTATUA TATIZO LA MADAWATI TANZANIA



Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Kayanza Pinda amesema shule za msingi nchini humo zinakaribiwa na upungufu wa madawati takribani milioni moja na nusu na akaitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipe kipaumbele suala la kupunguza tatizo hilo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo mwishoni mwa juma lililopita wakati akihutubia mamia ya wakazi wa mkoa wa Dodoma ambao walihudhuria uzinduzi wa wiki ya Elimu Tanzania kwenye uwanja wa Jamhuri .

Waziri Pinda alisema takwimu zinaonesha kuwa Tanzania inahitaji madawati 3,302,678 wakati madawati yaliyopo ni 1,837,783 kwa hiyo kuna upungufu wa madawati 1,464,895 katika shule za msingi.

Kutokana na mahitaji hayo Waziri Mkuu anasema kuwa endapo serikali itaamua kutengeneza madawati 100,000 kwa mwaka kwa gharama ya shilingi bilioni 12 itachukua miaka 15 kumaliza tatizo hilo ili kuziba pengo lililopo sasa.

Anasema ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe na serikali kumaliza tatizo hilo kwani inatia aibu na hakuna sababu ya kuendelea kuona wanafunzi wakisoma huku wamekaa chini.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.