MTANGAZAJI

ALBINO WAITAKA SERIKALI YA TANZANIA KUTUNGA SERA MAALUM YA MATIBABU YA KANSA YA NGOZI



Chama cha Albino Tanzania kimeita serikali ya Tanzania kutunga sera maalum ya kupambana na ugonjwa wa saratani ya ngozi,kwani mkakati uliopo sasa unaubaguzi kwa watu wenye ualbino.

Chama hicho kimetoa tamko hilo kupitia risala yake iliyosomwa na Mwakilishi wa Chama cha Albino Tanzania, Hussein Kibindo kwenye maadhimisho ya siku ya watu wenye ualbino iliyofanyika jana jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa saratani ya ngozi ni changamoto inayoongoza kwa kusababisha vifo kwa watu wa kundi hilo,hali inayosababisha watu wenye ualbino kuishi nusu umri tofauti na watu wengine.

Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kwenye maadhimisho hayo Waziri wa  Afya na Ustawi wa Jamii Dr Seifu Rashid amesema kuwa serikali itaendelea kufanya jitihada za kukabiliana na changamoto zinazolikabili kundi hilo ili kuhakikisha linapata haki ambazo linazozidai.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.