MTANGAZAJI

WATU 15 WAHOFIWA KULIWA NA MAMBA HUKO KIGOMA,TANZANIA



Zaidi ya watu 15 wakazi wa kijiji cha Chagu,kata ya Mtego wa Noti,Wilaya ya uvinza wanahofiwa kufa kwa kuliwa na mamba katika Bwawa la Mngonya liloko kilomo mkoani Kigoma.

Matukio hayo yameathiri shughuli za kijamii ,zikiwemo shughuli za uvuvi na kupunguza nguvu kazi ya kijiji hicho katika kata ya Mtego,hali iliyosababisha wanakijiji hao kutokuwa na imani na watendaji na viongozi wa idara husika kutokana na kufumbia macho tatizo hilo.

Katika hali isiyo ya kawaida baadhi wa wakazi wa kijiji hicho wamewaambia wanahabari kuwa ,  kufuatia ukimya huo wa muda mrefu wa watendaji na viongozi hali hiyo imewalazimu kufikisha kilio chao kwa mwenyekiti wa CCM mkoani Kigoma Daktari Walid Amani Kabouro.

Bwawa la Mngonya liloko Kilomo ni nguzo ya maendeleo kwa wananchi wa kijiji cha Chagu katika kufanikisha  shughuli za kijamii zikiwemo shughuli za uvuvi lakini inavyooneka wananchi hao wamekua wakiathiriwa na mamba walioko kwenye Bwawa hilo.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.