MTANGAZAJI

MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO MKOANI LINDI BADO NI TISHIO



Zaidi ya watoto 31 kati ya watoto 820 waliozaliwa mkoani Lindi kati ya kipindi cha mwaka 2013/2014 wamebainika kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa wazazi wao.

Hayo yameelezwa na Mganga mkuu wa Mkoa wa Lindi Daktari Yusuph Sonda katika uzinduzi wa huduma ya matumizi ya dawa Za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi (VVU) kwa wajawazito.

Daktari Sonda ameongeza kuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na shirika la Egpaf kupitia mradi wa kudhibiti ukimwi wameanzisha mpango mkakati wa kupunguza maambukizi ya ukimwi kutoka kwa mama kwende kwa mtoto toka asilimia 20 hadi asilimia tano.

Pamoja na juhudi zinazofanywa na wadau kuhakikisha huduma hizo zinapatikana,Mkoa wa Lindi bado unakabiliwa na changamoto  mbalimbli zikiwemo za  upungufu wa vituo vya kutolea huduma hizo hadi kufikia sasa kuna vituo 98 tu vinavyotoa huduma lakini hitaji la mkoa ni vituo 210.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.