MTANGAZAJI

WANANCHI MKOANI SHINYANGA WAITAKA SERIKALI KUTUMIA RASILIMALI ZA MADINI KUBORESHA SHULE



Wananchi Mkoani Shinyanga wameitaka serikali kutumia rasilimali za madini zilizopo kuboresha mazingira ya shule za msingi na sekondari kama nyumba za walimu vifaa vya kufundishia ili kupata walimu bora na wataalamu wenye ujuzi.

Wakizungumza na waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi hao,wamesema kuwa serikali inapaswa kufanya tathimini ya mafanikio yaliyopatikana kupitia migodi ya madini ya Buzwagi,Bulyanhulu na Mwadui katika kuchangia maendeleo ya jamii.

Licha ya serikali kujivunia mafanikio yaliyopatikana tangu uhuru kwa kuongeza sekondari kata,lakini shule hizo zinakabiliwa na matatatizo mengi.miongoni mwa matatizo hayo ni uhaba wa nyumba za walimu pamoja na maktaba za kisasa.

Mkoa wa shinyanga kupitia zao la madini linachangia zaidi ya asilimia kubwa katika pato la taifa lakini hali ambayo  haijasaidia kutoa ufumbuzi wa changamoto ya elimu mkoani humo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.