MTANGAZAJI

HALMASHAURI YA TEMEKE NA MKAKATI WA USAFI WA MAZINGIRA



Jumla ya watuhumiwa 172 walikamatwa na wengine  92 kupewa onyo kali na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam  katika  oparesheni ya usafi wa mazingira iliyoanza mwezi machi mwaka huu ili kuondoa kero za uchafuzi wa mazingira kwa makusudi katika halmashauri hiyo .

Taarifa ya Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke,William Muhemu aliyoitoa hivi karibuni kwa vyombo vya habari katika oparesheni hiyo watuhumiwa 80 walitozwa faini za papo kwa papo na kupatikana jumla ya shilingi  4,120,000 na wengine 45 walifikishwa mahakamani na kesi zao zinaendelea.

Katika operation hiyo jumla ya mabanda 415 na meza 2193 zilivunjwa na ombaomba 74 walikamatwa na kurudishwa makwao huku zoezi hilo lenye lengo la usafi wa mazingira,uzalishaji na utupaji ovyo wa taka ngumu na utumiaji wa vyoo likihusisha jumla ya nyumba 3614 na majengo ya biashara 225 yaliyokaguliwa.

Taarifa hiyo inaonesha kuwa kuwa ujenzi holela wa makazi, vyoo,ukosefu wa miundombinu kwenye makazi yasiyo rasmi na uhaba wa mabwawa ya maji machafu ni miongoni mwa mambo yanayochangia uchafuzi wa mazingira katika eneo la halmashauri hiyo .

Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ina ukubwa wa kilometa za mraba 656. Ina jumla ya watu 1,368,881 kwa taarifa ya sensa ya mwaka 2012.na tarafa 3 za Mbagala, Chang’ombe na Kigamboni. Pia ina kata 30 na mitaa 180. 


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.