MTANGAZAJI

WAKAZI WA UKEREWE MWANZA WAIOMBA SERIKALI KUDHIBITI WIZI WA MADAWA YA BINADAMU



Wakazi wa wilaya ya ukerewe mkoani Mwanza wameiomba serikali kudhibiti vitendo vya wizi wa madawa pamoja na vifaa tiba vinavyofanywa na baadhi na watumishi wa sekta ya afya ili kuwaondolea wananchi kero ya kuzitafuta huduma hizo katika maduka ya watu binafsi ambapo hakuna udhibiti wa bei.

Wakazi hao wametoa ombi hilo wakati wa ziara ya kamati ya utekelezaji ya jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi CCM mkoani Mwanza ambapo pia wametaka kukomeshwa wavuvi haramu vilivyo shamiri katika Ziwa Victoria.

Upatikanaji usioridhisha wa dawa katika baadhi ya zahanati na vituo vya afya mkoani Mwanza umeendelea kuwa kikwazo katika mapambano dhidi adui maradhi ambapo baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nduruma Wilayani Ukerewe wamehoji sababu ya zahanati ya kukosa dawa na kutakiwa kwenda kununua dawa kwenye maduka yanayomilikiwa na watumishi wa zahanati hiyo.

Hali hiyo imebainika wakati wa ziara ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Mwanza inayolenga kusikiliza kero za wananchi.

Kijiji cha Bukanda wananchi wamewasilisha maombi kutaka kukomeshwa kwa uvuvi wa kutumia zana haramu ulioshamiri katika ziwa Victoria.

         

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.