WAKAZI WA KIJIJI CHA GIBASO,TARIME WAMLALAMIKIA MWEKEZAJI
Wakazi wa kijiji cha Gibaso kilichoko
kata ya Nyarokoba Wilayani Tarime wamesema kuwa wanaitaji utaratibu ufuatwe dhidi
ya mwekezaji wanayedai kuwa amepora ardhi yao yenye zaidi ya hekari 2000 .
Uamuzi huo umefikiwa jana katika mkutano wa mkuu wa hadhara wa kijiji hicho uliowahusisha wana kijiji zaidi ya 300 chini ya Mwenyekiti wa Kijiji,Robert Morenda na Diwani wa Kata ya Nyarokoba Mustafa Masiani ambapo walidai kuwa kuchukuliwa kwa eneo hilo ni kuwataka wawe wakimbizi kwenye nchi yao hali ambayo itawafanya watahabike kimaisha kwa vile wana zaidi ya miaka 50 wakilima na kuishi eneo hilo.
Wamelitaja eneo hilo kuwa ni katika kitongoji cha Byantang'ana
linalopakana na kijiji cha Mrito kuwa limetaifishwa kwa kupewa mwekezaji Isack and sons co. ltd . huku wakisema kuwa mwekezaji huyo anadai kuwa anataka kuliendeleze eneo hilo kwa kulima zao la alizeti jambo ambalo si kweli.
Wamedai
kuwa wanachokiona wao eneo hilo kuna machimbo ya dhahabu ya Byantang'ana nakuwa
ndicho kinachomvuta mwekezaji huyo.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia shughuli za kusafisha eneo hilo zikiendelea huku wananchi wanaomiliki eneo hilo wakitakiwa kuondoka na mazao yao kukatwa na mkonge uking’olewa na kampuni hiyo..
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia shughuli za kusafisha eneo hilo zikiendelea huku wananchi wanaomiliki eneo hilo wakitakiwa kuondoka na mazao yao kukatwa na mkonge uking’olewa na kampuni hiyo..
Uchunguzi umebaini kuwa mgogoro huo uko
katika mahakama ya wilaya ya Tarime toka
mwezi wa kwanza mwaka huu, na inaonekana kuwa wizara ya ardhi nyumba na makazi imetuma barua
kwa wanakijiji hao ikionesha imemtuma mpimaji
Isack Marwa aliyetakiwa afike mwezi wa
nne mwaka huu katika kijiji hicho kupima eneo hilo.
Post a Comment