MTANGAZAJI

VIJANA WADOGO WA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO NJIRO ARUSHA KUTOA MAFUNZO KWA JAMII



Kanisa la waadventista wasabato mtaa wa Njiro jijini Arusha,kupitia idara ya vijana wadogo wa chama cha wavumbuzi na watafuta njia imeandaa mpango maalumu wa kuifanya jamii ya wakristo kurudi katika misingi ya maadili bora.

Mpango huu ambao utahusisha waadventista  na wasiowaadventista wasabato mkoani Arusha unatarajiwa kuwakutanisha vijana zaidi ya mia tatu na hamsini katika kanisa la Lemara ambapo watapatiwa mafunzo mbalimbali yanayohusu imani ya kweli pia namna ya kuwapelekea wengine Injili iokoayo.

Akizungumza na mwandishi wa habari Mchungaji  wa mtaa wa Njiro, Nuhu suleiman amesema kuwa Tukio hilo litakalofanyika may 17 2014 litawafanya vijana kujua na kutambua ni wapi misingi ya kijana mwenye maadili ilipo na ni kwa jinsi gani kuiendea. katika siku hiyo Vitabu zaidi ya mia mbili vya tumaini kuu vitasambazwa kwa watu mbalimbali katika maeneo ya lemara.

Kwa upande wake Youze Mangashi Kiongozi wa Idara hiyo ya vijana Mtaa wa njiro amesema Rali hiyo inalenga kuwaandaa na kuwahamasiha  vijana kwa ajili ya kambi kubwa conference ya kaskazini mashariki mwa Tanzania litakalofanyika Kwakoa mwezi wa sita mwaka huu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.