MAMA AMSAMEHE MUUAJI WA MWANAE WA PEKEE, NA SASA WANAISHI NYUMBA MOJA
Oshea akiwa amekumbatiana na mama wa marehemu |
Kwa hali ya kibinadamu ni vigumu kuamini ama kukubali kumsamehe mtu
aliyekutendea unyama wa ajabu ama jambo lililoondoa furaha yako lakini
pia kwa msaada wa Mungu jambo hili ni jepesi sana hasa kama Kristo
anatawala maisha yako. Mama mmoja aitwaye Mary Johnson's mkazi wa
Minnepolis nchini Marekani amemsamehe muuaji wa mwanae wa pekee na
kumkaribisha kupanga nyumba moja.
Muuaji huyo aliyefahamika kwa jina la Oshea Israel alimuua Laramiun Byrd
mwaka 1993 wakiwa katika sherehe ambako kulitokea mkwaruzano wa
kutoelewana na kijana huyo akijikuta akimuua mwenzake,
Mama huyo ambaye huimba mda wote afanyapo shughuli zake alimtambulisha
kijana huyo kwa mwenye nyumba yake mara baada ya kutoka jela mwaka 2010,
ambapo mwenye nyumba alikubali kumpangisha na sasa wanaishi nyumba moja
kama majirani na kushiriki kanisani pamoja, huku kijana huyo ambaye
kwasasa anamiaka 37 amekuwa akifanya kazi za kijamii kama kuomba msamaha
na kuonyesha fadhila kwa mama huyo. Lakini pia mama huyo kwasasa
ameanzisha kampuni iitwayo 'From Death to Life'
yenye lengo la kuhamasisha msamaha kati ya watu wahalifu na familia
zilizoguswa na watu hao. Hivi karibuni GK iliripoti habari ya familia
moja nchini Iran iliyoamua kumsamehe muuaji wa mtoto wao wa pekee,
ambapo bila hivyo ilikuwa muuaji huyo anyongwe hadharani mbele yao.
ambapo mama mzazi wa marehemu alishinikiza sheria kali ichukuliwe dhidi
ya muuaji wa mwanae ambaye kwa wakati huo alikuwa na miaka 16 alimuita
kuwa ni mnyama na anahitaji kifungo. Oshea alihukumiwa miaka 25 na nusu
jela pamoja na kutumikia jamii mara amalizapo kifungo chake.
Lakini miaka michache baadae mama huyo alianza kumtembelea kijana huyo
gerezani mara kwa mara na kujua namna msamaha unavyofanya kazi na
kukaririwa katika maongezi yake kwamba kutosamehe ni sawa na ugonjwa wa
kansa ambao utakutafuna ndani na nje hivyo ameamua kusamehe.
Chanzo:http://www.gospelkitaa.co.tz
Post a Comment