MAMA AMSAMEHE MUUAJI WA MWANAE WA PEKEE, NA SASA WANAISHI NYUMBA MOJA
|  | 
| Oshea akiwa amekumbatiana na mama wa marehemu | 
Kwa hali ya kibinadamu ni vigumu kuamini ama kukubali kumsamehe mtu 
aliyekutendea unyama wa ajabu ama jambo lililoondoa furaha yako lakini 
pia kwa msaada wa Mungu jambo hili ni jepesi sana hasa kama Kristo 
anatawala maisha yako. Mama mmoja aitwaye Mary Johnson's mkazi wa 
Minnepolis nchini Marekani amemsamehe muuaji wa mwanae wa pekee na 
kumkaribisha kupanga nyumba moja.
Muuaji huyo aliyefahamika kwa jina la Oshea Israel alimuua Laramiun Byrd
 mwaka 1993 wakiwa katika sherehe ambako kulitokea mkwaruzano wa 
kutoelewana na kijana huyo akijikuta akimuua mwenzake, 
 
Mama huyo ambaye huimba mda wote afanyapo shughuli zake alimtambulisha 
kijana huyo kwa mwenye nyumba yake mara baada ya kutoka jela mwaka 2010,
 ambapo mwenye nyumba alikubali kumpangisha na sasa wanaishi nyumba moja
 kama majirani na kushiriki kanisani pamoja, huku kijana huyo ambaye 
kwasasa anamiaka 37 amekuwa akifanya kazi za kijamii kama kuomba msamaha
 na kuonyesha fadhila kwa mama huyo. Lakini pia mama huyo kwasasa 
ameanzisha kampuni iitwayo 'From Death to Life'
  yenye lengo la kuhamasisha msamaha kati ya watu wahalifu na familia 
zilizoguswa na watu hao. Hivi karibuni GK iliripoti habari ya familia 
moja nchini Iran iliyoamua kumsamehe muuaji wa mtoto wao wa pekee, 
ambapo bila hivyo ilikuwa muuaji huyo anyongwe hadharani mbele yao.
ambapo mama mzazi wa marehemu alishinikiza sheria kali ichukuliwe dhidi 
ya muuaji wa mwanae ambaye kwa wakati huo alikuwa na miaka 16 alimuita 
kuwa ni mnyama na anahitaji kifungo. Oshea alihukumiwa miaka 25 na nusu 
jela pamoja na kutumikia jamii mara amalizapo kifungo chake.
Lakini miaka michache baadae mama huyo alianza kumtembelea kijana huyo 
gerezani mara kwa mara  na kujua namna msamaha unavyofanya kazi na 
kukaririwa katika maongezi yake kwamba kutosamehe ni sawa na ugonjwa wa 
kansa ambao utakutafuna ndani na nje hivyo ameamua kusamehe.
Chanzo:http://www.gospelkitaa.co.tz 

Post a Comment