MTANGAZAJI

SEKTA YA HABARI NA ELIMU ZAOMBWA KUKABILI CHANGAMOTO ZA MAZINGIRA NCHINI TANZANIA



Sekta ya habari na elimu zimeelezwa kuwa ni  nguzo imara ya kunusuru mabadiliko ya hali ya hewa na tabia ya nchi hapa nchini.

Hayo yamebainishwa na mtafiti wa mabadiliko ya hali ya hewa Dr Radisilaus Chang’a kutoka mamlaka ya hali ya hewa Tanzania 

TMA wakati akizungumza  na wadau katika semina  ya kujadili changamoto  ya mazingira kutoka wilaya ya Iringa vijijini.

Semina hiyo imelenga kuwaelemisha waandishi wa habari pamoja na walimu namna watakavyoielimisha jamii juu ya utunzaji wa mazingira ili kuendana na mabadiliko ya hali ya hewa hususani mkoa wa iringa

Radisilaus amewataka walimu wa shule za secondari mkoani Iringa kufikisha elimu ya mazingira kwa wanafunzi  wao ambao wanaweza kuisambaza elimu hiyo katika jamii inayowazunguka.

Pia ameiomba jamii kufuata maelekezo wanayoyapata kutoka kwa watalaam juu ya shughuli zao wanazozifanya hususani kilimo na matumizi ya nishati ya mkaa na kuni kwani kauli mbiu  ya mapambano hayo ni kata mti panda miti

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.