MTANGAZAJI

IRINGA:UPUNGUFU WA WAUGUZI WAKWAMISHA HUDUMA ZA AFYA



Imebainika kuwa Sekta ya afya mkoani Iringa  imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya idadi ndogo ya wauguzi na kusababisha wagonjwa kushindwa kupatiwa huduma muhimu na wakati mwingine kupoteza maisha kabla ya kuhudumiwa.

Mganga mkuu wa zahanati ya Ipogoro  Bw Andrea Mwinuka  amesema kuwa idara ya afya  mkoani Iringa inakabiliwa na changamoto hiyo, hivyo serikali itoe msaada ili kuondokana na tatizo hilo.

Aidha amewashauri wananchi kuendelea kuchangia mfuko wa jamii ili kupatikana fedha zitakazosaidia kununua dawa za kutosha ili kupunguza tatizo la ukosefu wa dawa.

Mkoa wa Iringa ni miongoni mwa mikoa inayokabiliwa na changamoto hiyo kwa baadhi ya hospitali na zahanati jambo ambalo linasababisha muuguzi mmoja kuhudumia wagonjwa wengi zaidi.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.