MTANGAZAJI

MAFURIKO YASABABISHA MAWASILIANO YA BARABARA KATI YA IFAKARA,MRIMBA MALINYI NA MAHENGE MOROGORO KUKATIKA







Mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini zimesababisha mafuriko katika mji wa ifakara mkoani Morogoro na kuharibu miundo mbinu ya barabara,madaraja na kivuko cha ifakara kwenda Mrimba mkoani humo.


Akizungumza na Morning Star Radio mmoja wa abiria waliokwama kwa siku nne kutokana na kukosa usafiri wa kuelekea  Mrimba kutoka mji mdogo wa  Mwembetogwa Ifakara,Mei Ibogo anasema sehemu kubwa ya barabara inayoelekea Mrimba imejaa maji na barabara hiyo haipitiki kwa sasa.


Anasema  ameshuhudia sehemu kubwa ya barabara kuelekea kivuko cha Mto Kilombero kinachovusha abiria kwenda  Malinyi  kutoka Ifakara imechukuliwa na maji na  hivyo abiria wanaoelekea mrimba na mahenge kukosa usafari kutokana na uharibifu huo.


Mei amesema yeye pamoja na abiria wengine wameshauriwa kusubiri maji ya pungue ama watumie usafari wa mitumbwi japo kwa wale wanaofahamu kuogelea kwakuwa maeneo mitumbwi hiyo inapita kumekuwa na changamoto ya kuzidiwa na maji na kupelekwa katika mwelekeo mwingine.  


Naye mkazi wa Mwembetogwa Khamisi Mumbira pamoja na kueleza kuwa mafuriko ya mwaka huu kuwa makubwa kuyashuhudia amesema usafiri ambao waweza kutumika sasa kutoka ifakara kwenda Mrimba ni treni ama trekta japo ameitupia lawama serikali kwa kutoshughurikia miundo mbinu ya barabara katika eneo hilo


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.