MTANGAZAJI

MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA AWATAKA WATANZANIA KUTOA USHIRIKIANO KWA VYOMBO VINADHIBITI MADAWA YA KULEVYA



Makamu wa Rais wa Tanzania  Dr Mohamed  Gharib Bilal amewataka watanzania kutoa ushirikiano kwa vyombo vinavyo shughulikia udhibiti wa dawa za kulevya ili wausika wachukuliwe sheria.

Dr Bilal ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru zilizozinduliwa leo Mkoani Kagera .Aidha amesema kuwa licha ya juhudi zinazofanywa bado tatizo la dawa za kulevya ni kubwa na kuwataka wananchi kuwataja waagizaji na wasambazaji wa dawa hizo ili wachukuliwe hatua.

 Dr.Bilal amewataka wananchi kujiepusha na vitendo vya kutoa na kupokea Rushwa vinavyochangia kuwanyima haki baadhi ya watu na kujiepusha na maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi.

Kuhusu mchakato wa katiba mpya Dr.Bilal amewataka wananchi kujitokeza kuipigia kura rasimu ya katiba mara Bunge maalumu la katiba litakapo kamilisha kazi ya kuijadili.

Kauli mbiu ya mbio za mwenge mwaka huu ni “katiba ni Sheria kuu ya Nchi jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba bora”.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.