MTANGAZAJI

VIFO VYA WATOTO KUTOKANA NA UGONJWA WA UKIMWI NI TISHIO NCHINI TANZANIA



Hatari  ya kuongezeka kwa vifo vya watoto vinavyotokana na ugonjwa wa Ukimwi na maradhi nyemelezi,inatishia taifa la Tanzania.

Hali hiyo inatokana na kuwapo idadi ndogo ya watoto wanaopata huduma na tiba ya ugonjwa huo kuwa chini ya asilimia 20 nchini humo.

Takwimu za shirika la Afya Duniani (WHO) za mwaka 2010 zinaonesha kuwa Tanzania ina watoto 230,000 wanaoishi na VVU na kati yao ni asilimia 26 pekee wanapata matibabu huku asilimia 74 ikikosa huduma hiyo.

Shirika la huduma za kichungaji kwa watoto wanaoishi na VVU mkoani Pwani na Dar es Salaam chini ya Kanisa Katoloki Jimbo Kuu la Dar es Salaam (Pasada), kwa kushirikiana na Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto Duniani (Unicef) wameanzisha mradi wa kupungunguza hatari hiyo.

Mkurugenzi wa ushauri na Utetezi wa Pasada na Meneja Mradi huo Jovina Tesha aliwaambia waandishi wa Habari hivi karibuni jijini Dar es Salaam mara baada ya Unicef kutembelea mradi huo  wa miaka miwili kuwa  malengo makuu ni kupunguza magonjwa na vifo kwa watoto wenye VVU.

Amesema kwa sasa wanatengeneza walimu watoto 120 kupitia klabu zetu 20 zilizopo jijini Dar es Salaam, nao watatoa elimu kwa watoto wenzao katika klabu na nyumba kwa nyumba na wakishawabaini, wanaohitaji tiba wataanza na wengine wataendelea kupewa huduma nyingine.

Mradi huo ulibuniwa Novemba mwaka jana na umeanza rasmi Januari mwaka huu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.