MTANGAZAJI

TAKUKURU YAELEZA SABABU ZA KUWEPO KWA RUSHWA



Imeelezwa kuwa mishahara midogo kwa wafanyakazi wa serikali na taasisi zingine,ubutu wa sheria mbalimbali,watu wasio waadilifu kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nyadhifa za juu pamoja na ukosefu wa vitendea kazi ni miongoni mwa sababu zinazo sababisha kuwepo kwa rushwa.

 Hayo yamebainishwa na afisa uchunguzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani iringa (TAKUKURU),Bw Akwilinusi Shiduki wakati alipokua akizungumza na mwandishi wa habari hii kuhusu wajibu wa vijana kupambana na adui rushwa.

Amesema vijana wanawajibu wa kutambua mchango wao katika kupambana na rushwa kama katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ibara ya 26,27 na 28 inavyosema,ambapo ameenda mbali zaidi kwa kusema sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa kifungu cha 39 kinatamka bayana kuwa kila mtu mwenye taarifa ya vitendo vya rushwa anawajibu wa kutoa taarifa hiyo kwa takukuru.

Shiduki amesema kuwa kuwepo kwa rushwa kunaweza kusababisha kushuka kwa pato la taifa,kuvusha nyara za serikali,madini na madawa ya kulevya,wananchi kukosa imani na serikali yao pamoja na kuwa na viongozi wasiofaa katika ngazi mbalimbali.

Sanjari na hayo afisa huyo amewataka vijana kuwa mfano wa kuigwa kwa kukataa na kukemea rushwa kila inapojitokeza na kuto shawishi kutoa au kupokea rushwa ili kupata au kutoa huduma kwa wanajamii au vijana wengine.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.