MTANGAZAJI

MAHAKAMA KUU YAMTIA HATIANI MKAZI WA NYAMAMONGO KWA KUJARIBU KUUA


Photo
Penina Magabe alivyosasa baada  ya kusikilizwa kesi ya kujaribu kuuwa 

Mahakama kuu mkoani Mara imemtia hatiani mkazi wa kijiji cha Nyamongo  Mwita Mwikwabe kwa kujaribu kuumuua Penina Magabe  mkazi wa kitongoji cha Nyichoka  Wilayani Serengeti.

Mwikwabe alitenda kosa hilo mapema  septemba 8, 2008 majira ya saa moja usiku kwa kumshambulia Penina kwa kumkata sehemu mbali za mwili wake kwa kutumia panga na hatimaye kukimbia kijijini hapo akihamia Kijiji cha Nyamongo Wilayani Tarime.

Mwendesha mashitaka wakili wa Serikali  Monica Hokororo na Valence Mayenga  waliiambia mahakama kuwa  mtuhumiwa baada ya kutenda kosa hilo alihamisha familia yake kwa kutumia lori aina ya fuso kwenda Nyamongo wilayani humo hata hivyo septemba 9, 2008 alikamatawa na jeshi la polisi na kurudishwa Wilayani Serengeti. 

Mwanasheria wa serikali Venance Myaenga amedai  kuwa Mwikwabe alitenda kosa hilo kwa kuvunja kifungu cha sheria ya adhabu namba 211(A) sura ya 16 kama ilivyorekebishwa mwaka 2012.
Na Waitara Meng'anyi-Tarime


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.