MTANGAZAJI

SERIKALI YAWATAKA WAKULIMA KUTOLIPIZA KISASI



Serikali wilayani Igunga mkoani Tabora imewataka wakulima wilayani humo kutolipiza kisasi cha mauaji kwa wafugaji wa wilaya kishapu mkoa wa shinyanga.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Igunga Bwana Elibariki Kingu wakati alipozungumza na wahanga wa tukio la mauaji ya wakulima watano wa wilaya ya Igunga baada ya kushambuliwa kwa mikuki na mishale na wafugaji wenye asili ya kitaturu kutoka wilaya ya kishapu mkoa wa shinyanga na kusababisha vifo vya wakulima watano wa wilaya ya Igunga. 

Aidha Bwana Kingu amewatupia lawama  baadhi ya wataendaji wa kata na vijiji kutofanya kazi zao kwa uadilifu na badala yake wamekuwa wakichukua rushwa kutoka kwa wafugaji na hivyo kusababisha wafugaji hao kufanya wanavyotaka.

 Machi 29 hadi 30 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili asubuhi katika wilaya ya igunga kulitokea mauaji ya wakulima watano na wengine kadhaa kujeruhiwa kwa wafugaji waliokuwa wakidai maeneo ya mashamba ya wakulima ni mali yao , hali iliyopelekea  mauaji hayo kutokea.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.