MTANGAZAJI

MKAKATI WA USAFI JIJINI ARUSHA

Wakazi wa jiji la Arusha wameipongeza serikali na manispaa ya jiji hilo kwa kutekeleza moja ya mikakati yake ya  kulifanya jiji kuwa safi na lenye hadhi ya miji ya kitalii hapa  nchini .


 Moja ya utekelezaji wa mikakati hiyo ni kuwaondoa wafanyabiashara wadogo wadogo waliokuwa wakiendea na biashara katikati ya mji na pembezoni  mwa Barabara,kubomoa vibanda na nyumba zote ambazo hazina hadhi ya kuwepo katikati ya mji ,huku lengo  ni kuhakikisha mpangilio bora wa nyumba zilizoko mjini.

     

Mpango huo umetekelezwa kufuatia amri iliyotolewa na mkuu wa wilaya ya Arusha Bwana John Mongela ya  kuwaondoa wafanyabiashara hao maarufu kama machinga wasifanye biashara zao katika maeneo yasiyoruhusiwa kisheria.


Kwa mujibu wa tathmini iliyofanywa na mwandishi wa habari hii  imeonyesha kuwa sheria na mpango huo umetekelezwa kwa asilimia tisini na tano huku waliokuwa wanategemea biashara hizo wakiwa hawana eneo maalum la kuendelezea shughuli zao za kila siku.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.