MTANGAZAJI

AJALI YASABABISHA VIFO MWANZA



Watu watatu wamefariki na wengine kujeruhiwa vibaya hadi kulazwa Hospitalini,kufuatia ajali mbili za magari zilizotokea jana na leo katika maeneo tofauto jijini Mwanza.


Leo, majira ya asubuhi huko Misungwi Mkoani Mwanza, watu watatu wamefariki na wengine ambao idadi yao haijafahamika wamejeruhiwa vibaya,kati yao wanne wamelazwa hospitalini hali zao zikiwa mahututi.


Ofisa Mwandamizi wa Makosa ya Jinai Mkoani Mwanza, aliyezungumza na Redio Morning Star Fm leo mchana, amesema ajali hiyo imetokea wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.


Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza,Valentino Mlowola kuzungumza kuhusu ajali hiyo hazikufanikiwa,kwa taarifa  kuwa alikuwa katika vikao.


Hata hivyo, habari  kutoka ndani ya jeshi la polisi zimesema,Kamanda Mlowola angetoa taarifa za ajali hiyo,baadaye alasiri  leo


Mpaka mwandishi wa habari hii anatuma taarifa hii waliokufa katika ajali hiyo,walikuwa hawajatambuliwa; na Kamaanda wa Polisi Mwanza alitarajiwa kutaja majina yao katika mkutano na wanahabari baadaye leo.


Wakati huo huo, ajali iliyotokea jana majira ya mchana katika eneo la Buzuruga,Nyakato jijini Mwanza ilisababisha watu kadhaa kupata majeraha na kutibiwa hospitalini.


Sababu za kutokea ajali za mara kwa mara jijini Mwanza zimetajwa kuwa ni mwendo kasi na uzembe wa madereva,hususan katika misongamano ya magari katika njia kuu za lami,ambako madereva huenda mwendo kasi pasipokuzingatia sheria za barabarani.

Na:Conges Mramba


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.