MTANGAZAJI

MEWATA KUFANYA UCHUNGUZI WA SARATANI KWA WANAWAKE JIJINI MWANZA



Chama cha Madaktari wanawake Tanzania(MEWATA)kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na taasisi zingine,kitazindua  Uchunguzi wa saratani ya Mlango wa Kizazi,Machi 8 mwaka huu jijini Mwanza.


Taarifa ya MEWATA iliyosainiwa na Mwenyekiti wake,Dk. Sarafina Mkuwa na kutolewa kwa vyombo ya habari hii leo jijini Mwanza inasema , zoezi hilo la uchunguzi kwa  akina mama wa Kanda ya Ziwa litafanyika katika uwanja wa Nyamagana kwa  siku mbili kuanzia Machi 8 hadi 9 mwaka huu.


Vituo vingine ambavyo zoezi hilo litafanywa ni Hospitali ya Nyamagana,Hospitali ya Wilaya ya Misungwi,Kituo cha Afya cha Misasi,Kituo cha Afya cha Buzuruga na Uwanja wa Shule ya Msingi Mirongo.


Mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa  Mke wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mama Salma Kikwete, ambaye pia ni   Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA).


Mama Kikwete  atakabidhi mashine 16 za kuchunguza saratani ya Mlango wa kizazi aina ya sikrotherapi (Cryotherapy) kwa waganga wakuu wa mikoa minne ya Mwanza, Mbeya,Iringa na Mara.


Haarifa zinasema kuwa Tanzania inaongoza  kwa wagonjwa wa maradhi hayo  Afrika Mashariki wakati kila mwaka wanawake 6,200 hugundulika kuathiriwa na maradhi haya,wakati kati yao wanawake 4,000 hufariki dunia kwa maradhi hayo

Hadi sasa kuna vituo 130 hapa nchini  vya kuchunguza saratani ya Mlango wa shingo ya kizazi katika mikoa 17.

 Na:Conges Mramba-Mwanza

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.