MTANGAZAJI

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA YATOA TAHADHARI YA KUNYESHA MVUA KUBWA



 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza uwezekano wa kunyesha mvua kubwa zinazoweza kuleta maafa katika baadhi ya mikoa ya Ukanda wa Pwani.


 Kwa mujibu wa taarifa ya tahadhari ya TMA iliyotolewa jana imeeleza  kuwa mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni pamoja na Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba mjini Zanzibar.


Taarifa hiyo inasema mvua hizo zinategemewa kunyesha kati ya Machi 05 hadi 07  mwaka 2014 na zitakuwa ni mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24, ikiwa ni kiwango cha wastani (65%).


Taarifa imefafanua kuwa hali hiyo inatokana na kuimalika kwa mgandamizo mdogo wa hewa mashariki mwa bahari ya Hindi sambamba na kusogea kwa haraka kwa mfumo wa mvua za msimu hivyo kuongeza kiwango cha unyevunyevu kutoka baharini kuelekea maeneo husika.


Hata hivyo Taarifa  hiyo imefafanua kuwa mvua zinazoendelea na zinazotarajiwa kunyesha zinaashiria kuanza mapema kwa mvua za masika katika baadhi ya maeneo ya pwani ya kaskazini ikiwemo Dar es Salaam,” imesema taarifa hiyo

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.