MTANGAZAJI

KATIBU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI NCHINI TANZANIA ASIMAMISHWA KAZI


Habari zilizoifikia blog hii jioni ya leo toka Dodoma zinaeleza kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo (pichani) amesimamishwa kazi. Akiongea na waandishi wa habari mjini Dodoma mapema leo, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, alisema kuwa Jairo amesimamishwa kazi kuanzia kesho ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili zilizotolewa bungeni mapema wiki hii. 

Ilielezwa wiki hii bungeni kuwa Jairo anatuhumiwa kuandika barua ya kuchangisha fedha milioni 50 kwa idara 20 ili zitumike kushawishi wabunge wapitishe bajeti ya wizara yake. Haijaelezwa amesimamishwa kwa muda gani.

1 comment

Anonymous said...

lazima tuwajibishane ili nchi ye2 ikae vyema,na sizani kama katibu huyu hii insue kaiunda pekee no!, da minister must be liable also,this is voracious liability,haijarishi katibu mkuu wa nishati na madini kafanya,ngereja lazima afate nyayo za katibu wake,afu tusitake sifa huyo mama mwacheni kabisaaaaaaaaaa,habari za kuwa katishiwa maisha hatutaki kuzisikia,tanzania ni ye2 sote,tumechoshwa na tabia za badhi ya watendaji,pamoja na serikali yake ,all in all kikwete totally filed hakuna jipiya usweiba unaiponza nchi ye2,utawabeba mpaka lin???????????????????,kila mbereko inachanika???????????????,watoto watodondoka vibaya hatimaye,bac sema inatoshaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mtazamo News . Powered by Blogger.