MTANGAZAJI

MBWA ANAPOKUA KITOWEO!!!!!!



Mkazi wa Kihesa katika manispaa ya Iringa akiendelea kumchuna ngozi mbwa aliyekuwa amegongwa na gari kwa ajili ya kwenda kumla kama kitoweo.
Tukio hilo la aina yake litokea majira ya jana saa 6 mchana katika eneo la kihesa Sokoni katika Manispaa ya Iringa ambapo mbwa huyo alikuwa amegongwa katikati ya barabara ya Kihesa Tumaini Iringa .
Kutokana na mzoga huu wa mbwa kubaki katikati ya barabara mkazi huyo ambaye alikuwa akinywa pombe ya kienyeji katika kilabu kimoja kilichopo jirani na eneo hilo alilazimika kunoa kisu chake na kumsogea mbwa huyo pembeni ya barabara na kuanza kumchuna ngozi huku akionyesha kuchekelea kuwa amepata mboga.
Kwa maelezo zaidi bofya hapa http://francisgodwin.blogspot.com/

3 comments

Anonymous said...

Wadau walaji nyama tuwe makini na nyama hizi la sivyo tutafakamia nyama ya wanyama ambao hata mungu hakutuagiza kuwala.Tukiendelea kwaw mtindo huu tutapata magojwa mengi sana!!

Anonymous said...

Huu ni ujinga wa huyu mzee si sifa anavyofanya dawa yake apate kipigo hapo, Hata kama kufa njaa si hivyo tena kuokota mizoga ya wanyama wasioliwa na kuwachuna njiani hadharani bora nile majani kuliko mzoga wa mbwa, halafu kwa nini asiuchukue sehemu ya mbali na watu akafanya anavyotaka au ni ushirikina huu, Pumbavu sana huyu mzee na ni mchavu wa kupindukia mi nikimuona nitampa kibano.

cat said...

be entertained

Mtazamo News . Powered by Blogger.