MTANGAZAJI

BALOZI KOMBO AKUTANA NA WADAU WA NGO JIJINI ROMA

 

  

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mahmoud Thabit Kombo amekutana na kufanya mkutano na wadau wa Taasisi zisizo za kiserikali (NGO) takribani sitini na nne zinazofanya shughuli zake nchini Tanzania mwishoni mwa juma Jijini Roma, Italia.

 Mkutano huo ulihudhuriwa pia na wadau mbalimbali wa Diaspora pamoja na wadau wa NGO walimpongeza Balozi kwa kuwapa nafasi ya kujitambulisha na kutoa fursa ya kuwasikiliza mafanikio yao sambamba na changamoto wanazopitia katika kufanikisha shughulika zao nchini Tanzania.
 
Pamoja na kuwasikiliza lakini pia Balozi alitumia nafasi hiyo kuwashauri kuwa na ushirikiano wa pamoja ili kuleta ufanisi zaidi kwenye maeneo wanayo yafanyia kazi. Aidha, katika mkutano huo Balozi Kombo aliongea mubashara na Balozi wa Italia nchini Tanzania  Mhe. Marco Lombardi na kumpa fursa ya kutoa salaam zake moja kwa moja kwa njia ya mtandao.
 
Balozi wa Italia nchini Tanzania aliwahakikishia wadau hao kuwa wapo kwenye mikono salama ya Balozi wa Tanzania Rome na chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Tanzania ni nchi salama ya kufanya shughuli zao.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.