MTANGAZAJI

RAIS KAGAME ASHIRIKI UZINDUZI WA CHUO KIKUU CHA AFYA CHA WAADVENTISTA (+VIDEO)


Rais wa Rwanda Mh,Paul Kagame akiwa sambamba na Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wasabato Ulimwenguni Pr.Teddy Wilson kwa pamoja wakisoma maandishi yaliyoandikwa kwenye jiwe la msingi,mara baada ya kuzinduliwa rasmi kwa chuo hicho leo mjini Kigali,nchini Rwanda.
Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wasabato Ulimwenguni Mch.Ted Wilson na Rais wa Rwanda wameshiriki katika uzidunzi wa Chuo Kikuu cha Afya nchini Rwanda kwa lengo la kutoa Elimu ya Afya kwa wanafunzi wa Afrika Mashariki na Kati

Hafla fupi ya uzinduzi wa chuo hicho cha afya kinachomilikiwa na Kanisa la Waadventista wa Sabato katika Divisheni ya Afrika Mashariki  na Kati (ECD) limefanyika Septemba 2 mwaka huu mjini Kigali ambapo Mch Ted Wilson amesema elimu bora siyo jengo bali ni huduma bora inayotolewa ndani ya majengo hayo huku akisema chuo hicho licha ya kutoa elimu ya afya inatoa huduma ya kiroho. 

Naye Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema kwa kutambua huduma mbalimbali zinazotolewa na kanisa hilo, Serikali yake itaongeza ardhi kwa chuo hicho pamoja na fedha, huku akipongeza Makanisa ya Waadventista wa Sabato nchini humo kwa kuadhimisha miaka 100 ya utoaji huduma ya kijamii na kiroho nchini Rwanda,kwani huduma walizozitoa zimekuwa na matokeo makubwa katika kuleta maendeleo hasa katika sekta ya afya na elimu. 

Awali akiwasilisha taarifa fupi ya chuo hicho Mwenyekiti wa jimbo la Afrika Mashariki na kati Mchungaji,Dkt  Blasous Luguri alieleza kuwa mpaka  kukamilika kwa ujenzi wa chuo hicho, kitasaidia kutoa mchango mkubwa wa elimu ya afya nchini humo. 

Uzinduzi wa chuo hicho umeshuhudiwa na viongozi wa Serikali ya Rwanda akiwemo Waziri wa Afya nchini humo Diana Lumba, Waziri wa Elimu Eugene Tamura pamoja na viongozi mbalimbali wa kanisa la Waadventista wasabato divisheni ya Afrika.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.