MTANGAZAJI

HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI-CHATO KUFUGULIWA JULAI 9,2019

 
 Waziri wa Maliasili na Utalii,Dkt Hamis Kigwangallah akizingumza wakati akifungua Mkutano Mkuu  baina ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA),Wahariri pamoja na Waandishi wa Habari Waandamizi ,Mkutano unaofanyika katika ukumbi wa mikutano katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza.

 

Waziri wa Malisili na Utalii ,Dkt Hamisi Kigwangallah amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  anatarajia kufungua rasmi Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato siku ya Jumanne ya Julai 9,2019 .

Dkt Kigwangallah ametoa kauli hiyo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka  baina ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ,Wahariri na Waandishi wa Habari Waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya Habari nchini ,mkutano unaofanyika jijini Mwanza.

Amesema Serikali inakamilisha mkakati wa kuanzisha utalii wa Majini katika maeneo ya Hifadhi na Vivutio vilivyopo ndani na Pembezoni mwa Ziwa Victoria "Boti Maalumu kwa ajili ya kusafirisha watalii kati ya maeneo ya Hifadhi zilizopo katika ukanda huu inatarajia kufika Mwanza hivi karibuni "alisema Dkt Kiwangallah .

Akimkaribisha Dkt Kigwangallah ,Kamishna wa Uhifadhi (TANAPA) Dkt Allan Kijazi amesema mkutano huo unafanyika kwa miaka sita mfululizo ni mkakati wa kuwawezesha wana habari kufahamu na kuelewa masuala ya Uhifadhi ili waripoti kwa usahihi mambo mblimbali yanayohusua Uhifadhi na Utalii kwa ujumla.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.