MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:HAKI ELIMU KATIKA UZINDUZI WA RIPOTI YA ELIMU KWA MIAKA 10 YA SERIKALI YA AWAMU YA NNE NCHINI TANZANIA

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2015/12/IMG_0221.jpg
Prof. Martha Qorro (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, John Kalage (kushoto) wakizinduwa ripoti ya Utafiti uliofanywa kuangalia hali ya utekelezaji wa ahadi na utoaji wa elimu hapa nchini katika kipindi cha miaka 10 ya serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete  jijini Dar es Salaam

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2015/12/IMG_0223.jpg
Prof. Martha Qorro (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, John Kalage (wa pili kushoto) wakionesha nakala za ripoti ya Utafiti uliofanywa kuangalia hali ya utekelezaji wa ahadi na utoaji wa elimu hapa nchini katika kipindi cha miaka 10 ya serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete
http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2015/12/IMG_0192.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, John Kalage akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya Utafiti uliofanywa kuangalia hali ya utekelezaji wa ahadi na utoaji wa elimu hapa nchini Tanzania katika kipindi cha miaka 10 ya serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete

Taasis ya HakiElimu hivi karibuni  imezinduwa ripoti ya Utafiti uliofanywa kuangalia hali ya utekelezaji wa ahadi na utoaji wa elimu hapa nchini katika kipindi cha miaka 10 ya serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa utafiti huo, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, John Kalage alisema ripoti iliyozinduliwa imeandaliwa na taasisi hiyo kwa ushirikiano na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Kitila Mkumbo, ambapo kwa ujumla imeangalia ubora wa elimu ya Msingi na ile ya Sekondari.

Alisema pamoja na mambo mengine ripoti iliyozinduliwa inaainisha changamoto zinazoikabili sekta hiyo na namna ya kukabiliana nazo. Alisema matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa Serikali ya awamu ya nne imefanya vizuri katika kupanua fursa za elimu kwa watoto wengi wa Kitanzania, bado kiwango cha elimu kimeshuka kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya Tanzania ikiwa huru.

"HakiElimu imekuwa na utamaduni wa kufanya tafiti zenye lengo la kutathmini, kuainisha na kuibua hari na changamoto za elimu nchini. Tumekuwa tukifanya tafiti za kila mwaka na tatifi za kipindi fulani kama hii. Lengo kuu ni kutuwezesha kuwa na taarifa hai juu ya maendeleo ya sekta ya elimu ili hata tunapoishauri serikali juu ya maeneo ambayo inapaswa kuboresha au maeneo ambayo imefanya vizuri, tuwe na ushaidi wa kutosha." alisema Kalage.

Akifafanua zaidi Kalage alisema kwa upande wa fursa za elimu katika kipindi cha miaka 10 ya JK kumekuwa na upanuzi mkubwa wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, ongezeko la idadi ya walimu, vitabu, udahili pamoja na kuhimarika kwa uwiano wa wasichana na wavulana wanaohitimu elimu ya msingi na sekondari.

"...Mathalani shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,538 mwaka 2015 huku wanafunzi shule za msingi wakiongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,202,892 shule za sekondari kutoka 1,745 mwaka 2005 hadi 4,753 mwaka 2015 huku idadi ya wanafunzi shule za sekondari wakiongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,804,056 mwaka 2015..." alisema Mkurugenzi Mtendaji huyo wa HakiElimu.

Aidha alisema katika kipindi hicho cha JK pia bajeti ya sekta ya elimu ilikuwa kubwa kuliko sekta nyingine yoyote ikiongezeka kutoka bilioni 669.5 mwaka 2005/2006 hadi shilingi trilioni 3.4 mwaka 2014/2015, upanuzi huo umewezesha asilimia 98 ya watoto wanaostahili kupata elimu ya msingi kujiandikisha. Kiwango cha udahili kwa shule za msingi pia kiliongezeka kwa zaidi ya asilimia 26 kwa ujumla, huku kiwango hicho kikiwa kikubwa zaidi kwa sekondari na elimu ya juu.

Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. Kitila Mkumbo akiifafanua ripoti hiyo alisema katika mambo ambayo Rais Kikwete alifanikiwa ni kupanua kiwango cha elimu ya Sekondari na vyuo vikuu jambo ambalo alisema endapo Rais Dk. John Pombe Magufuli akifuata vyayo zake Tanzania inaweza kufanya vizuri zaidi kielimu.

Alisema licha ya uwepo wa changamoto katika sekta hiyo suala la kuwekeza kwa walimu bora haliepukiki endapo Serikali itaamua kuboresha elimu nchini.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.