MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:BENJAMIN MKAPA ATAKA MFUMO WA UN UBADILISHWE

IMG_4995
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania Mh. Benjamin Mkapa akizungumza Kongamano la Umoja wa Mataifa lililofanyika jana jijini Dar es salaam katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.
IMG_7171
IMG_5045
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (kulia) akimpongeza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin Mkapa kwa hotuba nzuri.  Kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim akifuatiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe.
IMG_5544
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa kwenye kongamano hilo.
IMG_5619
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akitoa neno la shukrani kwa washiriki.

IMG_5630
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akisoma maneno yaliyoandikwa kwenye tuzo aliyokabidhi Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa. Kushoto ni Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Alvaro Rodriguez akijianda kukabidhi tuzo hiyo.
IMG_5644
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Alvaro Rodriguez (kushoto) akimkabidhi  Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa tuzo ya Umoja Mataifa  kwa kutambua mchango wake katika malengo ya millennia (MDGs) na kuwezesha Mashirika ya Umoja wa Mataifa kutoa huduma kama taasisi moja. Anayeshuhudia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe wakati wa Kongamano la Umoja wa Mataifa lililofanyika jana jijini Dar es salaam katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.
IMG_5661
IMG_5163
Mtandao wa vijana wanaopambana uharibufu wa mazingira (Youth Climate Activists Network), Fadhili Meta akiuliza swali Je Serikali inamikakati gani ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi?
IMG_5329
Mwanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Blesira Mukandala akitoa maoni yake kwa Umoja wa Mataifa ambapo aliuomba Umoja huo kuwatazama Walemavu kwa jicho la pili kama makundi mengine yanayofaidika na msaada wa mashirika ya Umoja huo.

IMG_5095
Pichani juu na chini ni Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania viongozi wa serikali, wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na wadau wa maendeleo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mdahalo huo.
IMG_7098
IMG_7118
Vijana pamoja na wanavyuo kutoka vyuo mbalimbali nchini wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea kwenye mdahalo huo.
IMG_7133
Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania pamoja na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na wadau wa maendeleo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mdahalo huo.
IMG_7151
Baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari nchini walioshiriki mdahalo huo.
IMG_7158
Ukumbi ukiwa umefurika wanafunzi, mabalozi, viongozi wa serikali, wanafunzi na wadau wa maendeleo wakati wa mdahalo kwenye juma la Umoja wa Mataifa ambalo linamalizika leo katika maadhimisho ya miaka 70 tangu kuundwa kwa umoja huo. Mdahalo huo umefanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jana.
IMG_7137
Maafisa kutoka UNESCO wakifuatilia mijadala mbambali iliyokuwa ikiendelea ukumbini hapo Kulia ni Nancy Kaizilege na Rehema Sudi (katikati).
IMG_7187
 Maafisa habari  na mawasiliano wa mashirika ya Umoja wa Mataifa Tanzania Jacqueline Namfua na Sawiche Wamunza wakifurahi jambo ukumbini hapo.
IMG_7221
Meza kuu katika picha ya pamoja na mabalozi waalikwa pamoja na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania.


Rais Mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania  Benjamin William Mkapa ametoa wito wa kufanyika kwa mabadiliko katika mfumo wa uendeshaji wa Umoja wa Mataifa ili kukidhi mahitaji ya sasa ya dunia.

Mkapa alisema hayo jana katika mdahalo kwenye juma la Umoja wa Mataifa ambalo linamalizika leo Oktoba 13,2015  katika maadhimisho ya miaka 70 tangu kuundwa kwa umoja huo. Mdahalo huo umefanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jana.

Mkapa ambaye alichukua muda wake mwingi kuelezea na kuangalia maslahi ya Umoja wa Mataifa kwa dunia na changamoto inazokabiliana nazo, alisema kwa muda sasa dunia inataka mabadiliko katika uendeshaji wa Umoja huo lakini wanaonufaika na mfumo wa sasa wamekuwa wagumu kukubali mabadiliko.

Alisema kuna mambo sasa yanatokea yanayohatarisha usalama wa mataifa, lakini hatua zinazopendekezwa zinashindwa kuchukuliwa kutokana na kuendelea kuwapo kwa tabia ya vita baridi kati ya mataifa makubwa yenye kura ya veto katika umoja huo.

Alisema yeye anaungana na watu wengine duniani wanaotaka mabadiliko katika Umoja huo yatakayozingatia jiografia za kisiasa duniani zinazoweza kusaidia kuinua uwezo wa utekelezaji wa Vyombo vya Umoja wa Mataifa likiwemo baraza Kuu na Baraza la Usalama.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.