MTANGAZAJI

MWANZA:ZAIDI YA WALIMU 2,000 WA MKOA WA MWANZA WANAIDAI SERIKALI YA TANZANIA


Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Gratian Mkoba


Walimu zaidi ya 2,000 mkoani Mwanza wanaidai serikali ya Tanzania  malimbikizo ya mishahara pamoja na gharama za upandishwaji madaraja.

 Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) mkoani Mwanza, Sibora Kisheri, amesema wanaungana na Rais wa chama hicho taifa, Gratian Mkoba kuitaka serikali kuwalipa madeni yao kabla ya Septemba mwaka huu.

Kisheri amesema kuwa baadhi ya walimu wanaidai serikali fedha za likizo na matibabu na wengine wakisubiri kupandishwa madaraja na kuongeza kuwa wanaunga mkono kauli ya Mkoba ya kuitaka serikali kulipwa madeni yao kabla ya Septemba mwaka huu pamoja na kwamba Rais Jakaya Kikwete alishaahidi kuwalipa wakati mkutano mkuu wa CWT uliofanyika mkoani Arusha.

Naye Katibu wa CWT Mkoa wa Mwanza, Said Mselem, ameiomba  serikali wakati wa kupanga bajeti, walimu wawe wanahusishwa ili inapopitishwa waelewe kilichopitishwa.

Mselem amesema CWT mkoa wa Mwanza hawatakubali kuona mwalimu yeyote mkoani humo anahamishwa na kupelekwa eneo jingine bila kulipwa gharama za uhamisho.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.